Afya

Mgonjwa wa Kifua Kikuu Akitibiwa Anapona kabisa?

“Daktari nina kikohozi cha zaidi ya wiki mbili sasa na nikikohoa makohozi yanatoka yaliochanganyika na damu, pamoja na kuchoka mwili, vilevile nikilala usiku natokwa na jasho sana”  Hiyo hapo juu ni nukuu ya maelezo ya mgonjwa mmoja alipoamua kufika hospitali baada ya kujaribu kutibu kikohozi kwa zaidi ya wiki mbili bila kupona, alizidi kuona hali […]

Mgonjwa wa Kifua Kikuu Akitibiwa Anapona kabisa? Read More »

Madhara ya kukaa muda mrefu kwenye kiti

“Kifo Kwenye Kiti”: Fahamu Hatari za Kukaa Muda Mrefu Sehemu Moja

Maisha ya kisasa yanawalazimisha watu wengi kukaa kwenye viti kwa saa nane au zaidi kila siku. Watu wengi hutumia muda mwingi wakiwa wamekaa. Wanafunzi hukaa darasani wakisoma, wafanyakazi hukaa ofisini, na wengi hukaa wakitumia simu au kompyuta. Ulimwengu tunaoishi sasa sio mkubwa kama ilivyokuwa zamani. Zamani watu walikuwa wakitembea kwenda sokoni, kulima, kuwinda, na kusafiri.

“Kifo Kwenye Kiti”: Fahamu Hatari za Kukaa Muda Mrefu Sehemu Moja Read More »

Kuna Athari Zozote za Kuongezewa Damu Mwilini?

Kama nilivyoeleza kwenye makala iliyopita (unaweza kuisoma kwa kubonyeza hapa), watu mbalimbali wanahitaji damu kwa mahitaji tofauti tofauti ikiwa ni pamoja na ujauzito, kufanyiwa upasuaji (operation) mkubwa, watoto kutokana na sababu mbalimbali, wagonjwa wa kansa, waliopata ajali na kupoteza damu nyingi kwa wakati mfupi, na kadhalika. Sio mara zote mtu anapatiwa damu yote kama ilivyotoka

Kuna Athari Zozote za Kuongezewa Damu Mwilini? Read More »

What happens during blood transfusion?

Nini Hutokea Mwilini Baada ya Kuchangia Damu? Kuna Faida Zozote?

Kumekuwa na kampeni nyingi za kuhamasisha watu kuchangia damu kwa hiari. Mara nyingi, mtu anapokuwa ana mgonjwa hospitali anayehitaji damu, ndugu wanahamasishwa kuchangia damu ili kuweza kurejesha ile ambayo mgonjwa wao amepatiwa.  Je, umeshawahi kujiuliza ni kwanini damu inahitajika kila siku? Na kuchangia damu kuna athari gani mwilini mwako?  Hali kadhalika mgonjwa wako anapopokea damu,

Nini Hutokea Mwilini Baada ya Kuchangia Damu? Kuna Faida Zozote? Read More »

effects of not sleeping well

Jinsi Usingizi Mdogo Unavyoleta Kitambi na Kuongeza Stress

Katika ulimwengu wa sasa wenye kasi, wengi wetu tunajivunia “kukesha.” Tunakesha tukifanya kazi (kumalizia kazi za ofisini), tukiangalia filamu (“episode moja ya mwisho”), tukicheza game au tukipita kwenye mitandao ya kijamii. Tumeanza kuuona usingizi kama anasa au dalili ya uvivu. Unakuta mtu anasema, “Nililala saa tisa alfajiri,” kana kwamba ni tuzo. Lakini, vipi kama nikikuambia

Jinsi Usingizi Mdogo Unavyoleta Kitambi na Kuongeza Stress Read More »

Nasumbuliwa na UTI Kila Mara, Nifanyeje?

Bila shaka swali kama hili sio geni kwako au inawezekana na wewe ni muhanga wa changamoto hii. Unapambana nayo vipi? Au unaishi nayo tu kama kawaida? Binafsi kama daktari nimekutana na wagonjwa wa namna hii mara kwa mara na nimekuwa nakijitahidi kutoa elimu ili kuhakikisha kila ninayekutana nae anapata msaada.   Kama wewe ni miongoni mwa watu ambao wanahisi UTI yao haiponi na inajirudia mara kwa mara basi usiache kusoma makala hii mpaka mwisho. Itakusaidia kupata njia sahihi ya kupita; njia namba tano itakushangaza.  Neno UTI ni kifupisho cha neno la kiingereza lijulikanalo kama Urinary Tract Infection, yaani maambukizi ya njia ya mkojo. Maambukizi haya, mara nyingi, husababishwa na bakteria mbalimbali

Nasumbuliwa na UTI Kila Mara, Nifanyeje? Read More »

Nikiungua Moto Nichukue Hatua Gani za Mapema?

Jamii ina utaratibu wake wa kufanya pale mtu anapoungua. Wewe unajua upi? Kwenye utamaduni wangu nimekuwa nikiona mtu akiungua anamwagiwa mkojo kwenye sehemu aliyoungua na imekuwa ikiaminika kwamba inasaidia.   Wengine huwa wanawahi kuweka asali sehemu iliyoungua wakiamini ni msaada mkubwa.  Wengine mafuta ya taa, petroli na kadhalika. Ninyi kwenu huwa  mnafanyaje?  Kuungua ni tukio

Nikiungua Moto Nichukue Hatua Gani za Mapema? Read More »

Madhara ya Kutomwambia Ukweli Daktari Wako

Mara nyingi tunapoenda hospitali hatusemi ukweli aslimia 100. Huenda unaogopa kumwambia daktari wako juu ya dalili zote ulizopitia, au muda ulioumwa, au kama umeshatumia mitishamba au dawa yoyote nyumbani kabla ya kwenda kumuona daktari.  Je, unajua madhara ya kutosema ukweli? Kunapoteza Muda Wako! Nimeshuhudia wagonjwa wengi wakipoteza muda hospitalini kwa kitu kidogo tu ambacho hawakusema

Madhara ya Kutomwambia Ukweli Daktari Wako Read More »

swSW